Thursday, November 12, 2015

BARAZA LA WANAWAKE WA CHADEMA (BAWACHA) MKOA WA RUVUMA WAMEMUOMBA MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA KUTENGUA UTAUZI WA ZUBEDA HASSAN SAKURU KUWA MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA RUVUMA


Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Ruvuma wamesema wanapinga vikali kuteuliwa Zubeda Hassan Sakuru kuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma.


Wanachama wa BAWACHA Baraza la Wanawake wa CHADEMA Mkoa wa Ruvuma wametoa Tamko la pamoja, wapo tayari kutoka CHADEMA endapo uteuzi huo hautabatilishwa  wamesema Zubeda Hassan Sakuru siyo mkaazi wa Mkoa wa Ruvuma hata wilaya waliyo sema ana toka Tunduru  hakuna hata mmoja anaye mjua . Jambo waliyo baini nikuona chama kipo mkononi mwa mtu mmoja.
 Wanawake wa CHADEMA kutoka wilaya za Tunduru, Nyasa, Mbinga, Namtumbo, Songea Vijijini na Songea Manispaa walipokutana katika Ofisi za CHADEMA wilaya ya Songea kutoa TAMKO hilo.
 Wajumbe wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Ruvuma (BAWACHA) wakiwa ndani ya Ofisi za CHADEMA wilaya walipokutana kwa ajili ya kutoa tamko la kupinga Uteuzi wa Mbunge wa Viti Maalum atakayewakilisha Mkoa wa Ruvuma uliofanywa na Uongozi wa CHADEMA Taifa.
 wanachama wa Chadema wakiwa nje ya Ofisi za CHADEMA wilaya Matarawe Manispaa ya Songea mara baada ya kutoa Tamko la Kupinga Uteuzi huo wa Mbunnge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma.

Baraza la Wanawake wa CHADEMA Mkoa wa Ruvuma (BAWACHA) wamemuomba Mwenyekiti wao wa CHADEMA Taifa Filiman Mbowe kubadilisha uteuzi alioufanya kumteua mtu ambaye hayuko katika Mkoa wa Ruvuma anaye tokea Tanga na kumteua kama mkazi wa Mkoa wa Ruvuma.

 Wanachama wa BAWACHA  nje ya Ofisi za CHADEMA wilaya ya Songea Mjini.

Wanawake wa Mkoa wa Ruvuma wa Chama cha CHADEMA wametoa siku tatu kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Filiman Mbowe kutengua Uteuzi wake wa kumuweka Zubeda Sakuru kuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Ruvuma wakati yeye ni Mwenyeji wa Mkoa wa Tanga na Ushahidi upo wa yeye kugombea Mkoa wa Tanga.



Wajumbe wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA Mkoa wa Ruvuma wameshangaa kuona hata Uongozi wa CHADEMA Mkoa wa Ruvuma hawakuonekana katika kikao kilicho andaliwa rasimi kupinga uteuzi wa Zubeda Sakuru na kudai uteuzi huo wa kumfanya Mbunge wa mkoa wa Ruvuma wamedai umetumika kulipa fadhila zinazo tiliwa mashaka.

Monday, November 19, 2012

SIKU 16 ZA UNYANYASAJI WA KIJINSIANCHINI TANZANIA

 Grece Mgambi Mwandishi kutoka inchini kenya akitafakari jinsi ya kuwaokoa wanawake wanao nyanyaswa kijinsia hapo Dar - es salaam ukumbi wa PeaCock Hotel
 Maurine Odwanga mwandishi kutoka nchini kenya ambaye ana fanya kazi katika gazeti la the Express akitafakari dhidi ya ukatili wa kijinsia
 Talibu Haule Mwandishi wa Ebon FM ya Iringa akiwa katika ukumbi wa peacock kujadili jinsi ya kuwapa uwezo wananchi wa vijijini
 Mahariri wa gazeti la Uhuru Shija akiwa ametulia kujipanga ili kuondoa mfumo dume katika Tanzania
 Fatuma Gafusi akitafakari jinsi ya kupeleka ujumbe kwa wanawake Dodoma ili kuepukana na ukeketaji wawanawake
 Yohana mtalamu wa kuandika makala akisiliza kwa makini mada kuhusu vitendo vya unyanyasaji wawatoto wakike
 washiriki wa semina ya unyanyasaji wa jinsia katika ukumbi wa Peacock jijini Sar -es -salaam
Gladiness mkufunzi wa kimataifa akiwa anajipanga tayari kuwakilisha mada kuhusu siku 16 za unyanyasaji wa kijinsia